Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Halima Okash ametoa siku 14 kwa wakurugenzi wote wa Bagamoyo na Chalinze kuyarejesha maeneo yote yaliohodhiwa na kuuzwa na viongozi wa vijiji kwa wawekezaji kwa maslahi yao binafsi na kuwa chanzo cha migogoro isiyokwisha.
Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Halima Okash ametoa siku 14 kwa wakurugenzi wote wa Bagamoyo na Chalinze kuyarejesha maeneo yote yaliohodhiwa na kuuzwa na viongozi wa vijiji kwa wawekezaji kwa maslahi yao binafsi na kuwa chanzo cha migogoro isiyokwisha. Pia, ameiagiza Taasisi ya Kupambana na Kuthibiti Rushwa (TAKUKURU) kufanya uchunguzi na kuwachukuliwa hatua za kisheria viongozi wote wa vijiji walihusika kuuza maeneo ya wafugaji yaliyopo katika mpango wa matumizi bora ya ardhi.