Mbunge wa Jimbo la Chalinze mkoani Pwani ambaye pia ni Naibu Waziri wa Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema Rais Samia Suluhu Hassan amewezesha kutoa fedha kutekeleza mradi wa maji wa Mdaula- Makondomengi unaokwenda kusaidia sana wananchi wa Chalinze na changamoto ya maji.
Mbunge wa Jimbo la Chalinze mkoani Pwani ambaye pia ni Naibu Waziri wa Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema Rais Samia Suluhu Hassan amewezesha kutoa fedha kutekeleza mradi wa maji wa Mdaula- Makondomengi unaokwenda kusaidia sana wananchi wa Chalinze na changamoto ya maji. "Mwenge wa Uhuru umekubali kuzindua mradi wa Maji Mdaula-Makondomengi wenye thamani ya Tshs. Milioni 344. Hatua hii ya Serikali inakwenda kutatua shida ya kipindi kirefu ya Maji ambapo wananchi walitembea zaidi ya Km 8 kufuata huduma ya maji na wengine wakitegemea Mabwana kwa maji ya Kunywa, na matumizi mengine. Asante Mhe. Rais Samia kwa kuendelea kuwajali Wanachalinze na Watanzania wenye uhitaji mkuu." Alisema Mhe. Ridhiwani Kikwete