Mon, 28 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Viongozi wa Mabaraza ya ardhi mkoani Kagera wametakiwa kutotegemea rushwa zinazokuwa zimebebwa kwenye mabegi na wananchi bali kufanya kazi kwa kufuata maadili na sheria ili kutenda haki na kutatua migogoro iliyopo.
Kauli hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Albert Chalamila wakati akiwaapisha wajumbe wa Baraza la Ardhi Wilaya Kyerwa ambapo amewataka kufuta sheria za nchi na kuepuka kupokea rushwa ili kutenda haki wananchi
Chalamila amesema, uapisho wa mabaraza haya nikutegemea matatizo yaliyopo ngazi ya kata na wilaya yamalizike huko kwa kuto haki ya kisheria kwa wananchi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live