Mon, 23 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bweni lililokuwa linatumiwa na wanafunzi zaidi ya 240 katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Umwani iliyopo Manispaa ya Bukoba, limeteketea kwa moto usiku huu.
Kwa mujibu wa Jeshi la Zimamoto hakuna mwanafunzi aliyedhurika na moto huo ulioanza majira ya saa 2:00 usiku. Uchunguzi kuhusu chanzo cha moto unaendelea.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live