Thu, 23 Sep 2021
Chanzo: Mwananchi
Mkazi wa jijini Dar es Salaam akiwa amebeba maboksi kufuatia kubomolewa kwa vibanda vya wafanyabiashara ndogo ndogo maarufu wamachinga katika eneo la Vingunguti jijini Dar es Salaam.Kazi ya kubomoa vibanda imefanyika usiku wa kuamkia leo.
Jana Septemba 22, 2021 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla ametumia ziara yake ya jimbo kwa jimbo mkoani humo kutoa elimu kwa wamachinga waofanya biashara zao katika maeneo yasiyo rasmi na kuhamia maeneo yaliyo rasmi.
Makalla amefanya hivyo ikiwa imepita siku tano tangu mkoa huo uzindue mwongozo wa kuwapanga wafanyabiashara hao.
Chanzo: Mwananchi