Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Bomba la gesi lazua taharuki Kilwa

82807 Pic+gesi

Tue, 5 Nov 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Kilwa. Shughuli zimesimama kwa muda wilayani hapa baada ya bomba la gesi asilia kuvujisha nishati hiyo katika kituo cha kupokea gesi cha Songas eneo la Songosongo na kusababisha muungurumo na moshi mkubwa uliowatisha wananchi.

Kutokana na hali hiyo magari yaliyokuwa yanayopita eneo hili yamelazimika kusimama huku ulinzi ukiimarishwa eneo la tukio kuzuia madhara yanayoweza kujitokeza.

Gesi hiyo inayovuja kwenye kituo hicho kinachomilikiwa na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) hivyo kuwashawishi walinzi wa kituo jirani cha kupokea gesi kutoka Madimba Mtwara na Songosongo kilicho chini ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) wakisaidia kuimarisha ulinzi.

“Ni kweli kuna hitilafu kidogo. Wataalamu wetu wanashughulikia hali hiyo ila hakuna moto wala madhara yoyote kwa binadamu,” amesema Nigel Whittaker mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Songas. 

Mkurugenzi huyo amesema walichofanya mpaka sasa ni kusimamisha uzalishaji wa gesi hiyo ili kurekebisha tatizo lililopo.

Kusaidia kudhibiti hali hiyo, gari la kikosi cha Zimamoto na Uokoaji limefika eneo la tukio lakini halifanyi chochote. Wananchi wapo kando wakishangaa kinachoendelea katika mradi huo.

Pia Soma

Advertisement

Chanzo: mwananchi.co.tz