Jeshi la Polisi mkoani Mbeya, limetangaza operesheni ya kuwakamata madereva wa pikipiki maarufu kama bodaboda wakataokuvunja sheria za usalama barabarani ikiwemo kupita kwenye taa za kuongoza magari bila kufuata utaratibu.
Mkuu wa Oparesheni wa Jeshi la Mkoa wa Mbeya, Abdi Issango ametoa kauli hiyo kwa niaba ya Kamanda wa Jeshi la Polisi, Ulrich Matei wakati akitoa elimu ya usalama barabarani kwa madereva hao.
Mkuu Kikosi cha Usalama barabarani Mkoa wa Mbeya, Yussuph Kamota amewataka madereva hao kuheshimu sheria za usalama barabarani.
Mwenyekiti wa Chama cha Madereva bodaboda Jiji la Mbeya, Aliko Fwanda alimehakikishia Jeshi la Polisi kwamba watazingatia sheria zote za usalama barabarani.