Wed, 16 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Madereva bodaboda wageukia fursa ya tatizo la maji “Maji ni dili kuliko abiria, nina mwezi sitaki abiria.”
Hizo ni kauli za madereva bodaboda wa Kinondoni Mosko jijini Dar Es Salaam walieleza jinsi tatizo la maji katika mtaa wao lilivyowapa fursa ndani mwezi mmoja na nusu.
Wamedai toka tatizo la maji lianze mwezi mmoja na nusu, biashara ya kusafirisha abiria wameliacha na kujikita kwenye kubeba maji na kuuza ambapo wamedai kwa siku wanauwezo wakuingiza Tsh 40,000.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live