Dar es Salaam. Mzee anayefahamika kwa jina la Hassan Abdallah Kitele (76) mkazi wa Tandika jijini Dar es Salaam anadaiwa kutoweka nyumbani kwake tangu siku saba zilizopita.
Akizungumza na Mwananchi leo Alhamisi Agosti 22, 2019 mtoto wa mzee Kitele, Fatuma Kitele amesema baba yake aliondoka nyumbani kwao bila kuaga Agosti 15,2019 asubuhi.
Fatuma amesema walipobaini baba yao hajarudi nyumbani kwa siku ya kwanza walianza kumtafuta bila mafanikio.
Ameeleza kuwa baadaye walitoa taarifa katika kituo cha polisi cha Chang’ombe jijini Dar es Salaam.
“Wakati anaondoka alivaa shati na suruali vyenye rangi ya kijivu, kofia ya blue na pia amekuwa akipoteza kumbukumbu mara kwa mara,” amesema Fatuma.
Mwanae huyo wa kike amesema tayari wameshafika kwenye vituo vya polisi mbalimbali, hospitali na shambani kwake Mkuranga mkoani Pwani alikokuwa anapaenda kutembelea huko kote hawajafanikiwa kumuona.
Pia Soma
- Kampuni ya Lindi Jumbo ruksa kuchimba madini ya Graphite
- Majeruhi ajali gari la Tanapa wahamishiwa Bugando, Arusha
- Tanesco yatoa sababu Kagera kutumia umeme wa Uganda