Sun, 9 Jan 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
"Mimi huwa naamka mapema saa11 au saa12 nakuja eneo hili kwa ajili ya kufanya usafi yaani kufagia. Nalipwa na hawa vijana walioko hapa. Kwa siku wananipa shilingi 200 au 300 naondoka.
Nyumbani niko na wajukuu wawili. Mimi sikuzaa ila ni wajukuu wa dada yangu ndio naishi nao" Ni maneno ya Bibi Mwajuma Ntemile mkazi wa Nangurukuru ambaye aliyazungumza na Team 360 hivi karibuni. Amepata fursa ya kuzungumza na Paul James @pjsweya na kuomba msaada kwa wasamalia wema waweze kumsaidia.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live