Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Benkiya NMB yatoa misaada ya milioni 17.3 kwa shule nne Mufindi

0 11 Benkiya NMB yatoa misaada ya milioni 17.3 kwa shule nne Mufindi

Mon, 19 Apr 2021 Chanzo: mtanzania.co.tz

Benkiya NMB imetoa misaada ya vifaa mbalimbali vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 17.3 kusaidia kuboresha upatikanaji wa huduma za jamii katika Wilayani Mufindi.



Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na madawati 50 kwaajili ya shule ya Msingi Upendo, Viti 12 na meza 12 kwaajili ya shule ya Isupilo na Mabati 200 kwaajili ya shule za msingi Nyamalala na Amani yenye lengo la kuezekea madarasa vyote vikiwa na thamani ya Sh milioni 17.3.

Baada ya kupokea misaada hiyo, Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Joseph Mchina, aliishukuru NMB kwa kuendelea kuchangia shughuli za maendeleo wilayani humo.

“Misaada hii imekuja wakati muafaka kwani itasaidia sana kupunguza uhaba wa madawati kwa shule zetu na pia kukamilisha baadhi ya madarasa ambayo yalikuwa ymameshajengwa lakini nguvu zilikuwa zinahitajika katika kuezeka, nawashukuru sana NMB,” aisema Mchina.

“Benki ya NMB imekuwa maili kwenye kuunga mkono juhudi za maendeleo za wananchi na kuisaidia Serikali kuboresha huduma za jamii. Naguswa na jinsi mnavyoe ndelea kutushika mkono sisi watu wa Mufindi na tunaomba msichoke kutusaidia,” alisema.

Mchina alisema kuwa ifike wakati wananchi waone umuhimu wa benki ya NMB katika kujitoa kwao na zawadi pekee ni kuwaunga mkono katika kufungua akaunti na kutumia benki hiyo kuweza kupata faida zaidi ili nao watoe zaidi kwa jamii katika sekta mbalimbali.

Meneja wa NMB Kanda ya Nyanda za Juu – Straton Chilongola aliushukuru uongozi wa wilaya kwa juhudi zake za maendeleo ya wananchi amba alisema ni wadau wakubwa kwa mafanikio ya benki ya NMB.

Alisema pia NMB inatambua mchango wa serikali kwenye kuisaidia kuweka mazingira wezeshi ya biashara wilayani Mufindi na hvyo na kwa mantiki hiyo nayo itaendelea kuwekeza kwa namna mbalimba ili kuwawezesha wananchi ambao ndio wadau wakubwa wa benki ya NMB kibiashara.

Aliongeza kuwa changamoto za sekta ya elimu na afya kwa NMB ni jambo la kipaumbele linalo hitaji kuunganisha nguvu kulikabiri.

“Ingawa Serikali inafanya makubwa, sisi kama wadau tuna wajibu wa kuunga mkono juhudi hizi za maendeleo kwa kusaidia jamii kwani kupitia jamii hiihii, ndio imeifanya Benki ya NMB kuwa hapa ilipo na kubwa kuliko benki yoyote hapa nchini.

“Sisi kama NMB tumekuwa mstari wa mbele kuchangia huduma za jamii kwa lengo la kurejesha sehemu ya faida yetu kwa jamii. Kwa zaidi ya miaka 10 mfululizo tumekuwa tukichangia asilimia moja ya faida yetu kila mwaka kama sehemu ya uwajibikaji kwa jamii inayo tuzunguka,” amesema Chilongola.



Wanafunzi washule zilizosaidiwa walisema msaada waliopata ni motisha tosha ya wao kufanya vizuri kitaa luma. Walimu wakuu wao walisema mchango wa NMB si tu nisehemu ya kurudisha fadhira kwa jamii lakini pia ni mchango mkubwa katika juhudi za kuboresha elimu nchini.

Chilongola aliongeza kuwa NMB inatambua juhudi za serikali kusimamia elimu na afya kwa nguvu zote kwa kutoa elimu bila malipo kwa shule za msingi na sekondari na kuboresha huduma za elimu na afya mjini na vijijini hivyo kama wadau kuna wajibu wa kuunga mkono juhudi hizo za maendeleo kwa jamii kwani ndio wameifanya benki ya NMB kuwa ilipo na kuwa benki kubwa kuliko zote nchini.

Meneja wa benki hiyo Tawi la Mafinga, Mary Mpasha alisema kuwa ushirikiano unaotolewa unasababisha biashara ya NMB kukua zaidi hivyo kufanya kama benki kuweza kutoa faida kwa jamii inayowazunguka kama benki bora nchini kwa sasa na yenye matawi mengi zaidi.
Chanzo: mtanzania.co.tz