Baraza la Wazee la Wilaya ya Kahama, limepaza sauti kupinga vitendo vya unyanyaswaji na mauaji ya wazee yanayoendelea kutokea katika baadhi ya maeneo duniani, huku wataalamu wa sekta ya ardhi wakiwashauri wazee na wanawake wajane kupima ardhi zao na kupata hati miliki kwa malengo ya kutatua migogoro ambayo imekuwa ikisababisha mauaji vikongwe ya mara kwa mara.
Baraza la Wazee la Wilaya ya Kahama, limepaza sauti kupinga vitendo vya unyanyaswaji na mauaji ya wazee yanayoendelea kutokea katika baadhi ya maeneo duniani, huku wataalamu wa sekta ya ardhi wakiwashauri wazee na wanawake wajane kupima ardhi zao na kupata hati miliki kwa malengo ya kutatua migogoro ambayo imekuwa ikisababisha mauaji vikongwe ya mara kwa mara. Wazee na uongozi wa baraza la wazee la Wilaya ya Kahama, wameyasema hayo wakati jopo la Wanasheria wanaoendesha kampeni ya huduma ya msaada wa kisheria ya Mama Samia Legal AID Campaign walipoungana na wazee wa Wilaya hiyo kusikiliza malalamiko yao, kama muendelezo wa siku ya wazee duniani.