Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe limepitisha mpango wa bajeti ya Sh67.6 bilioni kwa mwaka wa fedha 2023/2024
Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe limepitisha mpango wa bajeti ya Sh67.6 bilioni kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Akiwasilisha bajeti hiyo leo Januari 19, 2023 katika kikao cha Baraza hilo, Afisa mipango halmashauri ya wilaya ya Mbozi, Pantaleo Mkangara, kwa niaba ya Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Abdallah Nandonde, amesema bajeti hiyo inaongezeko la asilimia 3 ikilinganishwa na bajeti ya mwaka 2022/2023 ya Sh65.5 bilioni.