Sat, 23 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Zaidi ya Hekari 20 za dawa za kulevya aina ya Bangi zimefyekwa katika Kijiji cha Kewamamba kata ya Kiore wilayani Tarime mkoani Mara
Zoezi hilo limefanywa na jeshi la polisi kwa kushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama katika operesheni iliyofanyika hii leo ambapo mkuu wa wilaya ya Tarime Kanali Michael Mntenjele anasema kuwa zoezi hilo litakuwa endelevu.
Hata hivyo Mntenjele amewataka Wananchi kuachana na kilimo Cha Bangi na badala yake walime Mazao yanayokubalika.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live