Dae es Salaam. Serikali imependekeza kufuta tozo ya ukaguzi wa maduka ya vyakula na usajili wa maduka ya dawa za mifugo.
Wamiliki wa maduka ya vyakula walikuwa wanalipa Sh50,000 wakati waliotaka kusajili maduka ya dawa za rejareja za mifugo walitozwa kati ya Sh50,000 hadi Sh100,000.
Mapendekezo hayo yametolewa leo, Juni 13 na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alipokuwa anawasilisha bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2019/20 uliofanyika jijini Dodoma.
“Pia, naomba Bunge liridhie kufutwa kwa tozo ya ukaguzi wa viwanda vya samaki nchini ambayo ni kati ya Sh200,000 hadi Sh250,000 na tozo ya leseni ya mwaka ya biashara ya samaki iliyokuwa kati ya Sh50,000 hadi Sh300,000,” amesema Dk Mpango.