Tue, 12 Mar 2019
Chanzo: mwananchi.co.tz
Mbeya. Pikipiki za magurudumu matatu (bajaji) jijini hapa zimepigwa marufuku kutumia barabara kuu ya Mbeya-Zambia na dereva atakayekiuka hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
Kauli hiyo ilitolewa jana na ofisa mfawidhi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchikavu (Sumatra) Nyanda za Juu Kusini, Denis Daudi katika kikao cha mamlaka hiyo, wamiliki na madereva wa bajaji.
Daudi alisema ni katazo la Jiji la Mbeya kwa bajaji kutumia barabara kuu kibiashara na katazo la kubeba abiria kutoka nje ya jiji. (Yonathan Kossam)
Chanzo: mwananchi.co.tz