Tue, 3 Aug 2021
Chanzo: millardayo.com
NI Simanzi na Majonzi kwa wakazi wa Loliondo baada ya kutokea kwa kifo cha Babu wa Loliondo alifariki Julai 30, 2021.
Sasa leo Agosti 3, 2021 Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro, Raymond Mwangwala amesema Mwili wa Mchungaji Ambikile Mwasapile maarufu kama Babu wa Loliondo unatarajiwa kuzikwa Agosti 4, 2021 katika Kijiji cha Samunge huko Ngorongoro mkoani Arusha.
Babu wa Loliondo alifariki kwa maradhi ya kuugua Nimonia kali iliyompa changamoto ya upumuaji na kupelekea umauti.
Chanzo: millardayo.com