Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

BREAKING: Watano wafariki kwenye ajali ya magari matatu kwa mpigo

Screenshot 2021 06 21 At 20.32.37 660x400.png BREAKING: Watano wafariki kwenye ajali ya magari matatu kwa mpigo

Tue, 22 Jun 2021 Chanzo: millardayo.com

Watu watano wamefariki kwenye ajali iliyotokea usiku huu eneo la nanenane mkoani Morogoro na kuhusisha magari matatu ambayo ni Basi dogo aina ya Toyota Coaster, Lori na gari dogo aina ya Toyota Cresta.





Kamanda wa Polisi Morogoro Fortunatus Muslim amesema chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa Dereva wa Coaster kutaka kuyapita magari yaliyopo mbele yake bila kuchukua tahadhari akitokea Dar es salaam kuelekea Mbeya kuzika akiwa amebeba mwili wa Marehemu pamoja na Abiria.



Kamanda Musilimu amesema hadi sasa bado haijafahamika idadi ya majeruhi lakini miili ya wote waliofariki ambao ni Wanaume watatu na Wanawake wawili imepelekwa Hospitalini. 
Chanzo: millardayo.com