Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Askofu Kasala akitaka chuo cha Saut kujitathimini

65174 Pic+askofu

Tue, 2 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Mwanza.  Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC),  Flavian Kasala amekitaka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustine kutumia miaka 20 ya kuanzishwa kwake kama kioo cha kujitathimini kule walikotoka na wanakoelekea.

Amesema kujitathimini huko kujikite katika masuala yote ya kiutendaji ikiwemo suala la kutoa elimu na la kiroho kama lilivyo lengo la chuo hicho.

Akihubiri katika misa takatifu leo Jumanne Julai 2, 2019 ibada iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kiserikali akiwemo Rais mustaafu wa awamu ya tatu wa Tanzania,  Benjamin Mkapa, Askofu Kasala amesema mtu yeyote asiyefanya tathimini hawezi kujua mwelekeo wa maisha yake na wakati mwingine anajikuta anafanya mambo yasiyompasa kufanya.

"Katika maisha ya kawaida ni lazima ufanye tathimini ili uweze kufanya vitu vya heshima kwa kuwasamehe waliowakosea, kupongezana na kukosoana," amesema  Askofu Kasala

Katika hatua nyingine, amekitaka chuo hicho kuangalia kisije kukumbwa na mambo ya kidunia na kujikuta wakijikita katika kutoa elimu pekee na kusahau masuala ya kiroho.

"Tutumie miaka 20 kufanya tathimini na kutafakari utendaji wetu na  kumshukuru Mungu kwa watu wote waliochangia kuhakikisha chuo kimefika hapo kilipo," alisema Kasala

Pia Soma

Askofu Kasala ambaye pia ni Askofu wa Jimbo la Geita amewataka wasikatishwe tamaa na changamoto zilizotokea huko nyuma bali washikamane pamoja na kila mmoja awe faraja kwa mwenzake katika kufikia malengo yao.

Amesema chuo hicho kimekuwa kituo cha muungano wa  makabila na mataifa mbalimbali na kimefanikiwa kuhitimisha zaidi ya watu 30, 000 ambao wengi wamerudi chuoni hapo kutoa shukrani.

Endelea kufuatilia Mwananchi kujua kinachoendelea katika sherehe hiyo

Chanzo: mwananchi.co.tz