Thu, 17 Dec 2020
Chanzo: habarileo.co.tz
JESHI la Polisi mkoani Pwani limewataka abiria kutoa taarifa ya madereva wanaokiuka sheria za usalama barabarani na kusababisha ajali.
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufanya operesheni ya kukagua mabasi yanayokwenda mikoani, magari ya mizigo na magari madogo kituo cha mabasi cha Maili Moja, Mlandizi na Vigwaza,
Kamanda wa Polisi mkoani humo, Wankyo Nyigesa alisema kuwa wameamua kufanya hivyo ili kubaini mabasi na magari ambayo yana matatizo ili yasiwepo barabarani na kusababisha ajali.
Chanzo: habarileo.co.tz