Serengeti. Makoye Matondo (50), mkazi wa kijiji cha Bukore Wilaya ya Serengeti amelazwa hospitali ya Nyerere wilayani humo baada ya kujeruhiwa na tembo.
Akizungumza leo Jumatatu Oktoba 7, 2019 mganga mkuu wa hospitali hiyo, Tanu Warioba amesema Matondo alifikishwa katika hospitali hiyo jana Jumapili.
Ofisa wanyamapori wa Wilaya hiyo, John Lendoyani amesema Matondo alikuwa anatoka katika sherehe na akiwa njiani alikutana na mnyamapori huyo na kumjeruhi.
"Alijeruhiwa kwenye nyonga tumeishawataarifu hasa walioko pembezoni mwa maeneo ya hifadhi kuepuka kutembea usiku bila tahadhari maana ni kipindi ambacho tembo wanatembea sana kutafuta malisho," amesema.