Sun, 10 Jul 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkazi wa Kijiji cha Kapanga wilayani Tanganyika, Heleni Nyankole maarufu Beberu (36), anayedaiwa kuwa kinara wa kufanya mauaji ya kukodiwa, ameuawa kwa kupigwa risasi.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 10, 2022, Kamanda Polisi Mkoa wa Katavi, ACP Ally Makame (Pichani) amesema mtuhumiwa huyo aliuawa usiku wa kuamkia leo wakati wa akipambano na polisi.
Kamanda Makame amesema kuwa mtuhumiwa huyo anadaiwa kukodiwa kufanya mauaji ndani ya Mkoa wa Katavi na nje ya mkoa huo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live