Thabo Bester maarufu kama Mbakaji wa Facebook ambaye ni Raia wa Afrika Kusini aliyetoroka Gerezani kwa kughushi kuwa amefariki amekamatwa Jijini Arusha Tanzania.
Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania David Misime amethibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo akiwa na Mpenzi wake Dr. Nandipa Magumana pamoja na raia mwingine Zakaria Alberto
Misime amesema taratibu za mawasiliano ya kisheria ya ndani na ya kimataifa zinaendelea kukamilishwa
Thabo alighushi kuwa amefariki kwa kujichoma moto alipokuwa gerezani lakini baadaye ikabainika kuwa hajafariki bali ametoroka na Polisi wakaanzisha msako wa kumtafuta
Mtuhumiwa huyo alikuwa gerezani kwa makosa mbalimbali huku kubwa ikiwa ni kuwarubuni Waathiriwa kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook kisha kuwabaka na kuwaibia ambapo