Unguja. Wananchi na askari na maofisa wa Polisi tayari wamefika katika Msikiti wa Kibweni kwa ajili ya kuisalia maiti ya aliyekua kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Aziz Mohamed Juma.
Mohammed ambaye amefariki dunia leo Jumapili Juni 9, 2019, maiti yake imekutwa ikining’inia kando ya nyumba yake na atazikwa makaburi ya Mwanakwerekwe yaliyopo mjini hapa.
Wananchi wengi wanaonekana kuwa na huzuni na kushindwa kuamini kilichotokea baada ya taarifa za kifo kuelezwa kuwa ni za kujinyonga.
Awali, Kamanda wa Polisi Zanzibar, Mohamed Hassan Haji aliliambia Mwananchi kuwa kifo cha ofisa huyo si cha kawaida.
Hata hivyo, alisema licha ya uwapo wa tetesi kuwa amejinyonga nje ya nyumba yake huko Kijichi, lakini alisema hawezi kueleza kwa kina taarifa hizo kwa sasa kwa sababu bado mapema.
Alisema wanachokifanya sasa ni uchunguzi na wakibaini sababu watatoa taarifa.
Pia Soma
- Waziri atoa msimamo mradi wa gari za umeme mlima Kilimanjaro
- Tuzo ya hifadhi ya Serengeti kupelekwa kwa Rais John Magufuli
- Viongozi wa upinzani Sudan wakamatwa
Tayari zilichukuliwa sampuli za damu kwa uchunguzi zaidi.