Serikali imesema itaendelea kuuthamini na kuuenzi mchango wa wazee walioshiriki katika tukio la kihistoria la kuchanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar.
Serikali imesema itaendelea kuuthamini na kuuenzi mchango wa wazee walioshiriki katika tukio la kihistoria la kuchanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar. Hayo yamesemwa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Khamis Hamza Khamis, wakati akitoa salamu za serikali katika mazishi ya Mzee Hasanieli Mrema aliyeshiriki katika tukio la kuchanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar, katika Kijiji cha Mdawi wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro Mei 08, 2024.