Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Akutwa na alama za Barabarani za Tsh milioni 10 ndani

Alama Za Barabarani Akutwa na alama za Barabarani za Tsh milioni 10 ndani

Tue, 20 Feb 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Jeshi la Polisi mkoani Tabora linamshikilia jamaa aliyefahamika kwa jina la Moshi, kwa tuhuma za uharibifu na wizi wa alama za usalama barabarani kutoka katika barabara mbalimbali katika mkoa huo baada ya kukutwa na alama zenye thamani ya zaidi ya Sh. milioni 10 nyumbani kwake.

Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari Kamanda wa Polisi, ACP Richard Abwao, amesema mtuhumiwa huyo alikamatwa saa 12 asubuhi katika Kata ya Usege wilayani Kaliua.

Amesema walimkamata mtuhumiwa huyo baada ya kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema ambao wanapiga vita vitendo vya uharibifu wa alama za barabarani.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live