Sun, 7 Mar 2021
Chanzo: www.habarileo.co.tz
Mkazi wa Kijij cha Kanazi Kata ya Ntantubila wilaya ya Nkasi mkaoni Rukwa, Deus Kakusu (52) amejinyonga hadi kufa, kwa madai ya ugumu wa maisha.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, William Mwanampangale athibitisha mkasa huo na kudai kuwa mtu huyo alitumia chandarua cha mbu kujinyonga ndani ya jiko nyumbani kwake katika kijiji hicho cha Kanazi.
Mwenyekiti wa kijij hicho cha Kanazi, John Kebevage alisema marehemu amechukua uamuzi huo mgumu wakati mke na watoto wake wakiwa wamelala.
Chanzo: www.habarileo.co.tz