Mtu mmoja amefariki dunia baada ya lori alilokuwa akiendesha kupoteza mwelekeo na kutumbukia katika daraja la Mto Tegeta kwa Ndevu, Kinondoni Dar es Salaam.
Mtu mmoja amefariki dunia baada ya lori alilokuwa akiendesha kupoteza mwelekeo na kutumbukia katika daraja la Mto Tegeta kwa Ndevu, Kinondoni Dar es Salaam. Akizungumza nasi, Mrakibu wa Polisi, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kinondoni, Peter Mtui ameseme chanzo cha ajali hiyo iliyotokea leo alfajiri ni mwendo kasi wa madereva wa malori hayo waliokuwa wakikimbizana, hivyo kusababisha mmoja kupoteza mwelekeo na kuvunja kingo za daraja na kutumbukia mtoni.