Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ajali ya mwanafunzi, mwalimu asimamishwa kazi

Mwalimu Simamishwa (600 X 418) Ajali ya mwanafunzi, mwalimu asimamishwa kazi

Thu, 5 Oct 2023 Chanzo: mwanachidigital

Mwalimu Furaha Msule anayefundisha Shule ya Sekondari Kidegembye iliyopo Lupembe Halmashauri ya Wilaya ya Njombe amesimamishwa kazi kwa kosa la kuwachukua Wanafunzi na kuwapeleka kupakia kuni zake kinyume na sheria na kupelekea kupata ajali ya gari wakati wakirudi majira ya saa moja usiku.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Christopher Sanga amethibitisha kusimamishwa kazi kwa Mwalimu Msule na kutoa wito kwa Watumishi kufanya kazi kwa kufuata sheria kanuni na taratibu.

"Ofisi ya Mkurugenzi kwa kushirikiana na Tume ya Walimu imechukua hatua ya kumsimamisha kazi Mwalimu aliyehusika huku utaratibu, sheria na kanuni nyingine zikiendelea"

Sanga amesema October 01,2023 ofisi yake ilipokea taarifa ya kutokea kwa ajali ambapo Mwalimu Furaha aliwachukua Wanafunzi na kwenda kupakia kuni zake lakini kwa sasa Wanafunzi wote 11 wakiwemo 6 waliokuwa wakitibiwa katika Hospitali ya Kibena wameruhusiwa na kurejea Shuleni.

Chanzo: mwanachidigital