Mon, 22 Aug 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Lori la mafuta limeanguka hii leo Jumatatu, Agosti 22, 2022, wilayani Gairo mkoani Morogoro, huku ikielezwa kwamba baadhi ya wananchi wamefika katika eneo la ajali na kuanza kuchota mafuta.
Tukio hili linakuja ikiwa ni miaka mitatu tangu ajali kama hiyo itokee na kuua zaidi ya watu 100 katika eneo la Msamvu, Morogoro Mjini, mnamo Agosti 10, mwaka 2019.
Askari waliofika katika eneo hilo ili kuzuia umati wa watu wasikimbilie kuchota mafuta na kuepuka athari za vifo vinavyotokana na mlipuko wa malori ya mafuta.
Taarifa kamili zitafuata.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live