Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Abiria wasotea usafiri Moshi

32967 Magaripic Tanzania Web Photo

Sat, 22 Dec 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Moshi. Abiria wanaosafiri kutoka Moshi kwenda maeneo mbalimbali leo Jumamosi Desemba 22, 2018 wamekumbana na adha ya usafiri kutokana na ongezeko la abiria wanaokwenda kusherekea sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya.

Wengi waliokwama mjini Moshi mkoani Kilimanjaro ni wanaoelekea mikoa ya Tanga na Singida, hali iliyosababisha  nauli kwenda Tanga kupanda kutoka Sh13,000 hadi Sh15,000.

Mwananchi limeshuhudia uwepo wa msongamano mkubwa wa abiria kituoni hapo kwa wale wanaoingia na kutoka.

Pia, limeshuhudia  abiria wengi  wakiwa wamekaa maeneo tofauti huku baadhi wakizunguka kusaka usafiri.

Ashura Juma, anayesafiri kwenda jijini Tanga amesema tangu asubuhi amefika kituoni hapo lakini magari mengi yamejaa.

Mmoja wa wakatisha tiketi kituoni hapo, Valerian Msuya amesema abiria wanaokwenda Tanga wamekuwa wengi kupita kiasi na wanakosa mabasi.

 “Tangu jana abiria wanaosafiri kwenda Tanga wamekuwa wengi, hawa wote unaowaona hapa wanaenda Tanga lakini ndio hivyo magari yanajaa mapema na hakuna msaada mwingine labda kama yatakuja magari mengine baadaye ”amesema Msuya.

Hivi karibuni, Ofisa Mfawidhi wa Mamlaka ya Udhibiti, Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra), Johns Makwale alisema 2018 wamejipanga kuhakikisha  changamoto zilizojitokeza mwaka 2017 hazitajirudia tena kwa kutoa vibali kwa magari binafsi yenye uwezo wa kubeba abiria 50 kusafirisha abiria maeneo mbalimbali.

 

 



Chanzo: mwananchi.co.tz