Lindi. Abiria wawili waliokuwa wakisafiri na basi la Buti la Zungu kutoka Dar es Salaam kwenda Mtwara nchini Tanzania wamenusurika kifo baada kula biskuti zinazodaiwa kuwa na dawa za kulevya wakiwa ndani ya basi hilo.
Abiria hao ni Dadi Rashid (49) ambaye ni ofisa elimu taaluma Utete wilaya ya Rufiji mkoa wa Pwani na Omary Burian (27) mfanyakazi wa bodi ya korosho Dar es Salaam.
Akizungumzia tukio hilo leo Jumatano Novemba 27, 2019 Kaimu mganga mfawidhi Hospitali ya Sokoine mkoani Lindi, Idrisa Chande amethibitisha kuwapokea wagonjwa hao jana usiku Jumanne wakiwa hawajitambui na kwamba wanaendelea na matibabu hospitalini hapo.
Kamanda wa polisi mkoa wa Lindi, Poudence Proteus amesema amepokea taarifa hiyo na atalizungumzia baada ya uchunguzi kukamilika leo Jumatano.