Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Abiria finyu wasitisha safari za mabasi Dodoma kuelekea Morogoro, Dar es Salaam

97801 Abiria+pic

Wed, 4 Mar 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Baadhi ya mabasi ya abiria katika stendi kuu ya mabasi Dodoma yanayofanya safari kupitia mkoani Morogoro yameshindwa kufanya safari leo Jumanne, Machi 3, 2020 baada ya kukokosa abiria.

Hatua hiyo imekuja baada ya kukatika kwa daraja katika barabara kuu ya Dodoma-Morogoro eneo la Dumila mkoani Morogoro.

Akizungumza na Mwananchi leo, Katibu wa Mawakala wa Mabasi Stendi Kuu Dodoma (Ummdom), Yahaya Iddi  amesema magari hayo hayajafanya safari leo kutokana abiria wengi kuahirishwa safari.

Iddi amesema mabasi hayo yaliahirishwa safari kwa kupitia kupata hasara kwa kupitia barabara ya mkoa wa Iringa-Morogoro baada ya kuona abiria walikuwepo ni wachache baada ya wengi kuahirisha safari.

"Mabasi yanayotokea hapa stendi kuu hayajafanya safari leo, abiria walikuwa wachache na walivyokuja hapa wamewaambia hali ilivyo wapo baadhi waliamua kurudi nyumbani na wengi wanatumia magari yanayotokea Singida, Tabora au mikoa ya Kanda ya Ziwa,"alisema Yahaya.

Hata hivyo, amesema magari ya kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa jana yalilala jijini Dodoma na leo asubuhi yaliendelea na safari kwa kupitia mkoani Iringa.

Alisema yale yenye vituo maalumu katikati ya jijini la Dodoma yameendelea na safari kama kawaida kwa barabara ya Iringa, Morogoro badala ya Dodoma Morogoro.

Mmoja wa abiria anayeenda Dar es Salaam, Joyce Geremia amesema alifika stendi tangu asubuhi lakini hajafanikiwa kupata usafiri.

Amesema alichoambiwa ni kusubiria magari yanayotoka mikoa ya Singida au Tabora kwa gharama ya Sh35,000 badala ya Sh20,000.

Chanzo: mwananchi.co.tz