Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wazee wamkaribisha Maalim Seif kuwania uraisi kupitia Chadema

16799 Pic+chadema TanzaniaWeb

Tue, 11 Sep 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Wazee wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema kipo tayari kumkaribisha Katibu Mkuu wa CUF, Seif Sharif Hamad kuwania urais kupitia chama hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Septemba 11 Mwenyekiti wa Wazee wa Chadema, Hashimu Juma amesema kutokana na mgogoro unaoendelea CUF,wameona kuna kila sababu ya Maalim Seif kuhamia Chadema.

Wazee hao wamesema wameshafanya naye (Maalim)mazungumzo ya awali.

Pamoja na mambo mengine wamesema hakuna sababu ya kufanyika chaguzi za mara kwa mara kutokana na kujiuzulu kwa viongozi hasa wabunge na madiwani.

Mwenyekiti huyo wa Taifa amesema gharama za chaguzi hizo zinatokana na kodi za wananchi.

Chanzo: mwananchi.co.tz