Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watendaji wa vijiji wafunga ofisi, wagombea washindwa kurejesha fomu

Watendaji wa vijiji wafunga ofisi, wagombea washindwa kurejesha fomu

Thu, 7 Nov 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Arusha. Chama cha demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mkoa wa Arusha kimelalamikia wagombea wake katika uchaguzi mdogo wa serikali za mtaa  zaidi ya 100 kushindwa kurejesha fomu baada ya watendaji wa vijiji na Kata kufunga ofisi tangu asubuhi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Novemba 4, 2019, Katibu wa Chadema Mkoani Arusha, Elisa Mungure amesema jitihada za kuwatafuta viongozi hao tangu asubuhi zimekwama katika vijiji vingi vya wilaya za Arusha, Arumeru, Monduli, Longido na Karatu.

"Tumeandika malalamiko yetu kwa wasimamizi wa uchaguzi lakini hatujui hatma yake, hivyo tunaomba wanahabari mtusaidie kufikisha hizi taarifa ili watu wajue rafu tunazochezewa,” amesema Mungure.

Amesema licha ya watendaji kufunga ofisi, baadhi ya wagombea wameporwa fomu zao, wengine wamekamatwa na kundi la  vijana.

“Huu si uchaguzi, ni vurugu wenzetu CCM wagombea wao wamejaza fomu na kupelekwa majumbani kwa watendaji wa vijiji na Kata ili kuhakikisha wagombea wa upinzani hawarudishi fomu,” amedai Mungure.

Katibu wa Chadema wilayani Arusha, Innocent  Kisanyage  amedai kuwa mgombea wa nafasi ya mwenyekiti katika  Mtaa wa Masikiria Kata ya Terrati, Justine Laizer alivamiwa juzi usiku na na watu waliodaiwa kuwa ni polisi.

Chanzo: mwananchi.co.tz