Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wapinzani wataka Bunge kujadili sintofahamu uchaguzi Serikali za mitaa

83173 Pic+wabunge

Fri, 8 Nov 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Baadhi ya wabunge wa upinzani leo Jumatano Novemba 6, 2019 wamelitaka Bunge la Tanzania kusitisha shughuli zake ili kujadili hali ya sintofahamu iliyojitokeza wakati wa kurejesha fomu za uchaguzi wa Serikali za mitaa.

Vyama vya upinzani vimelalamikia ukiukwaji wa kanuni na kufanyiwa hujuma zilizosababisha kuenguliwa kwa wagombea wao wengi kwenye mchakato wa uchaguzi huo.

Uchaguzi wa Serikali za mitaa utafanyika Novemba 24, 2019 na hatua ya uchukuaji fomu kwa wagombea ilimalizika Novemba 4, 2019.

Nafasi zinazowaniwa ni mwenyekiti wa kitongoji, mwenyekiti wa kijiji, mwenyekiti wa mtaa, wajumbe wa halmashauri ya kijiji na wajumbe wa kamati ya mtaa.

Waliozungumzia sintofahamu hiyo bungeni leo ni  Maftaha Nachuma (Mtwara Mjini), Magdalena Sakaya (Kaliua), Frank Mwakajoka (Tunduma) na  Anatropia Theonist

Mwakajoka amesema kinachoendelea kuhusu uchaguzi huo kinaweza kusababisha machafuko na uvunjifu wa amani kama Serikali haitakuwa makini.

Habari zinazohusiana na hii

Advertisement
Anatropia amesema wapinzani wanalia nchi nzima kutokana na mambo mbalimbali wanayofanyiwa na kushangazwa na agizo la Waziri wa Tamisemi, Seleman Jafo kutofanyiwa kazi. Jafo aliagiza wagombea walioenguliwa bila sababu za msingi kurejeshwa.

Maftaha amesema wana vielelezo vya kanuni zilizokiukwa katika uchukuaji wa fomu za uchaguzi huo na kuomba avikabidhi kwa Spika wa Bunge, Job Ndugai ili chombo hicho cha Dola kisitishe shughuli zake, kujadili uchaguzi huo.

Akijibu miongozo hiyo naibu spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson amewataka wabunge kuwa wavumilivu kwa maelezo kuwa Jafo alishatoa maelekezo yanafanyiwa kazi.

Chanzo: mwananchi.co.tz