Dodoma. Waziri Kivuli wa Kilimo nchini Tanzania, Pascal Haonga amesema bajeti ya maendeleo katika sekta ya kilimo hairidhishi, kwa miaka mitatu mfululizo imetolewa kidogo.
Akizungumza bungeni mjini Dodoma leo Jumatano Februari 5, 2020, Haonga ambaye pia ni mbunge wa Mbozi (Chadema) amesema utekelezaji wa bajeti unasuasua ikiwa imepita imeshapita nusu ya mwaka.
Amesema mwaka 2019/2020 bajeti iliyotengwa kwa ajili ya maendeleo katika kilimo ilikuwa ni Sh143.5bilioni lakini zilizotolewa hadi sasa ni Sh21.4bilioni.
Amesema licha ya fedha hizo kutolewa kidogo kiwango kinachotoka kwa wafadhili ni kikubwa kuliko kinachotolewa na Serikali.
“Utekelezaji umekuwa wa tabu sana na wa kusuasua. Hali ni mbaya,” amesema Haonga.
Ameitaka Serikali kulipa madeni yanayodaiwa na wakulima wa pamba na korosho nchini ili kuwawezesha kuendeleza kilimo nchini.
Pia Soma
- Mbunge CCM ataka wabunge kukatwa posho wapewe mawaziri, amtaja Lugola
- Mvua Dar yavuruga soko la ‘mahakama ya ndizi’
- Afa akizungumza na simu iliyokuwa kwenye chaji
Amesema bei elekezi ya mbolea hiyo ni Sh54,000 lakini hivi sasa inauzwa kati ya Sh64,000 hadi Sh70,000.