Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wanasiasa watakiwa kuwa wakweli

Mabuline Dkt Mabula yuko mkoani Mbeya

Mon, 9 May 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amewataka wanasiasa nchini kuwa wakweli wakati wa kutekeleza majukumu yao ili kuepuka kuleta migongano baina ya Serikali na wananchi.

Dkt Mabula ametoa kauli hiyo mkoani Mbeya wakati Kamati ya Mawaziri wa Wizara za Kisekta ilipokutana na uongozi wa mkoa na wilaya kwa lengo la kutoa mrejesho wa Maamuzi ya Baraza la Mawaziri kuhusiana na utatuzi wa migogoro ya matumizi ya ardhi katika vijiji 975.

‘’Tusitafute kura kwa kudanganya wananchi halafu mwisho wa siku tunakosa maneno mazuri ya kuwaambia kutokana na kuwaaminisha kuwa ukiwa kiongozi hawataondoka eneo fulani hivyo kupatwa na kigugumizi utaenda kusema nini wakati ushawaaminisha’’ alisema Dkt Mabula.

Kwa mujibu wa Waziri Dkt Mabula, wanasiasa wanatakiwa kuwa wakweli kwenye masuala ambayo ni kwa ajili ya ulinzi, maendeleo na mustakabali wa nchi na kama kuna makosa yalifanyika huko nyuma kwa kusajiliwa vijiji maeneo ya hifsadhi basi wakaeleze ukweli na na kusisitiza serikali haiko tayari kurudia makosa.

Akigeukia uamuzi wa serikali kuhusu vijiji 975, Dkt Mabula alisema serikali ya mkoa wa Mbeya inalo jukumu la kusimamia utekelezaji wa uamuzi wa Baraza la Mawaziri kwa kushirikiana na taasisi na mamlaka zote zilizopo ndani ya mkoa.

Mkoa wa Mbeya unahusisha vijiji/Mitaa 58 yenye migogoro ya matumizi ya ardhi ambapo vijiji 31 kati ya hivyo vitabaki kwenye maeneo yake huku vijiji/ mitaa 21 wataalamu wakifanyia tathmini na kutoa mapendekezo ya namna ya kutatua migogoro iliyopo kwa manufaa ya Taifa.

‘’Nitoe angalizo maeneo yote ambayo wataalam wanafanyia kazi serikali imekwisha chukua picha za anga za maeneo husika hivyo hatutegemei kuona shughuli mpya zikifanyika katika maeneo yote ambayo wataalam wanapita’’ alisema Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live