Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetangaza majina 11 ya wanachama waliojotokeza kuchukua fomu kuwania nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwa ni siku 12 tangu kufunguliwa mchakato huo.
Akitaja majina hayo katika Makao Makuu ya Chama hicho ,Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa chama hicho ,Tumaini Makene amewataja kuwa ni pamoja na watu 11 waliotia nia Urais Chadema, Isaya Mwita, Tundu Lissu, Peter Msigwa, Wakili Nikodemus Gaspar, Naro Opio.
Wengine ni Wakili Richmund Simba, Lazaro Nyalandu na Shabani Msafiri, Dkt Majinge Maryrose, Manyama Leornard na Freeman Mbowe