Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wakazi waliopisha Uwanja wa ndege Dodoma kulipwa kesho

16736 Pic+dom TanzaniaWeb

Tue, 11 Sep 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Wakazi wa Dodoma waliopisha upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Dodoma, wataanza kulipwa kesho.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Atashasta Nditiye amesema kila kitu kimekamilika hivyo hakuna sababu ya kulalamika.

Nditiye ametoa kauli hiyo bungeni leo septemba 11, 2018 wakati akijibu swali la nyongeza la mbunge wa viti maalumu Ferista Bura (CCM).

Mbunge huyo ametaka kujua ni lini wananchi wa Dodoma ambao nyumba zao zilivunjwa na kuwekewa alama ya X kwa ajili ya kupisha ujenzi na upanuzi wa uwanja wa ndege.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz