Thu, 18 Apr 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini, Mwita Waitara amesema Rais Samia Suluhu Hassan ataendelea kusemewa mazuri kwa sababu ni mama mwenye nyumba aliyefanya maendeleo makubwa katika kila sekta, jambo ambalo ni kazi kubwa.
Waitara amesema hayo Bungeni jijini Dodoma wakati akichangia Bajeti ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa mwaka wa Fedha 2024/2025 Bungeni jijini Dodoma.
“Tusipomsema mama Samia unataka tumseme nani? Yaani tuache kumsemea Mwenyekiti wetu tukuseme wewe kwa lipi?... Unataka tuseme nini? Mama Samia anatosha na chenji inabaki,” amesema Waitara.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live