Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Vyama vyaungana na CUF kudai mikutano ya hadhara

69802 Cuf+pic

Mon, 5 Aug 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Chama cha Wananchi (CUF) kimeviibua vyama vingine vya siasa baada ya kumuomba Rais John Magufuli aruhusu mikutano ya hadhara ikiwa imebaki miezi miwili kabla ya uchaguzi wa viongozi wa Serikali za Mitaa.

Mikutano hiyo ilipigwa marufuku mwaka 2016, miezi michache baada ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu, kwa maelezo kuwa siasa hufanywa wakati wa uchaguzi.

Viongozi walioshinda katika Uchaguzi Mkuu ndio walioruhusiwa kuitisha mikutano katika maeneo yao, lakini amri hiyo imekuwa ikipingwa na viongozi wa kisiasa ambao wanasema inakiuka Katiba na Sheria ya Vyama vya Siasa.

Viongozi hao pia wanalilaumu Jeshi la Polisi kwa kutosimamia vyema amri hiyo kutokana na kuwabana wapinzani pekee.

Huku uchaguzi wa viongozi wa Serikali za Mitaa ukipangwa kufanyika Oktoba, CUF ilitoa ombi hilo kwa waandishi wa habari jana na mara moja vyama vingine vikaiunga mkono ambavyo ni Chadema, ACT-Wazalendo, Chaumma, NCCR-Mageuzi huku Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM (Uhusiano wa Kimataifa), Kanali Ngemela Lubinga akisema uchaguzi ukikaribia mikutano hiyo itaruhusiwa.

“Tunaiomba Serikali kutoa tamko la kuruhusu mikutano ya hadhara wakati huu wa maandalizi ya kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa,” alisema Salvatory Magafu, mkurugenzi wa sheria na haki za binadamu wa CUF, alipozungumza na waandishi wa habari.

Pia Soma

Alisema mikutano ya hadhara ni muhimu kwa ajili ya viongozi kuzungumza na kusikiliza kero za wananchi, hivyo ni muda muafaka kuiruhusu kuanzia muda huu wa kuandikisha wapigakura.

“Tunamuomba Rais John Magufuli atoe tamko la kuruhusu mikutano ya hadhara kwa kuwa alipopiga marufuku aliahidi kuruhusu kipindi cha uchaguzi hivyo huu ni muda muafaka,” alisema Magafu.

 

Kwa habari zaidi soma gazeti la Mwananchi la leo Jumapili Agosti 4, 2019

Chanzo: mwananchi.co.tz