Mhariri wa Jarida la Afya Mwananchi Communications Ltd, Herieth Makwetta amesema kwa mujibu wa takwimu za afya, takriban watu 850 wamefika kwenye vituo mbalimbali vya afya na kubainika kuwa na maambukizi ya ugonjwa wa macho mekundu 'Red Eyes'
Awali ugonjwa huo ulioanza Dar es Salaam lakini baadaye ukasambaa katika mikoa mingine.
Kuna haja ya kujipanga kutoa elimu kabla ya majanga. Wakati mamlaka ya hali ya hewa ilipotangaza uwepo wa mvua za El Nino Wizara ya Afya pamoja na wizara inayohusika na masuala majanga zilipaswa kujipanga kuhakikisha kwamba mvua hizo haziwezi kuleta maafa.
Wizara husika zina jukumu la kujipanga kuhakikisha maafa kama hayo hayatokei ili tusije kufika kule ambako wenzetu wa Malawi walifika.
Ameyasema hayo leo alipokuwa akichangia mjadala wa Mwananchi X Space katika mada isemayo 'Tufanye nini kuzuia magonjwa ya milipuko?'