Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

‘Viongozi wa CCM tokeni mkabaini changamoto zinazowakabili wananchi’

Thu, 30 May 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Unguja. Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kusini Unguja, kimewataka viongozi na watendaji wake ngazi ya matawi na majimbo kufanya ziara za mara kwa mara kwenye taasisi za Serikali ili kubaini changamoto zinazokwamisha upatikanaji wa huduma bora kwa wananchi ili zitafutiwe ufumbuzi.

Wito huo umetolewa leo Alhamisi Mei 30, 2019 na Mwenyekiti wa CCM Wilaya hiyo, Abdulaziz Hamad Ibrahim katika mwendelezo wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM, katika vituo vya afya kwenye Jimbo la Paje Unguja.

Alisema endapo viongozi wa ngazi hizo wataendeleza utamaduni wa kufanya ziara hizo, itasaidia kupunguza changamoto zilizopo kwenye sekta mbalimbali za utoaji huduma kwa wananchi.

Alisema kupitia ziara hiyo ya siku mbili kwenye vituo vya afya vya majimbo ya Makunduchi na Paje, imesaidia kubaini  changamoto zinazokwamisha upatikanaji wa huduma za afya.

Alisema CCM inatekeleza Ilani yake ya Uchaguzi ya Mwaka 2015/2020 kwa ufanisi zaidi ili kuhakikisha wananchi wa mijini na vijijini wanapata huduma kwa viwango vinavyostahili.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, maofisa utabibu wa vituo hivyo vya afya, waliipongeza Serikali Kuu kwa kufanya ugatuzi ambao  umeongeza upatikanaji wa huduma bora kwa wananchi hususan wa vijijini.

Pia Soma

Ziara hiyo ya Kamati ya Siasa ya Wilaya  imefanyika katika vituo vya afya vya Paje, Bwejuu, Michamvi na Mungoni.

Chanzo: mwananchi.co.tz