Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Vikao vya Bunge vinavyoanza kesho kuendeshwa kidijitali

Vikao vya Bunge vinavyoanza kesho kuendeshwa kidijitali

Thu, 7 Nov 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Bunge litaanza kutumia Bunge Mtandao katika Mkutano wa 17 unaoanza kesho jijini ambao utapunguza gharama zilizokuwa zikitumiwa na mhimili huo kwenye uchapishaji wa nyaraka mbalimbali kutoka Sh 1.2bilioni hadi Sh 200milioni kwa mwaka.

Akizungumza leo Jumatatu Novemba 4, 2019 baada ya maelekezo kwa wabunge kuhusu matumizi ya Tablets (Vishikwambishi), Katibu wa Bunge Stephen Kigaigai amesema mfumo huo utaokoa fedha zilizokuwa zikitumiwa na Bunge pamoja Serikali.

“Wizara zinazohusika tumezitaka zije na karatasi kiasi kwa ajili ya kumbukumbu za ofisi. Kwa maana ya maktaba na baadhi ya maeneo kwa hiyo kwa kesho tunaanza Mpango wa Serikali nadhani tutakuwa na nakala ambazo hazitazidi 10 zamani walikuwa wakileta nakala 500, ”amesema kigaigai.

Kigaigai amesema wamenunua Tablets 450 zenye  thamani ya zaidi ya Sh900 milioni ambazo zitagawiwa kwa wabunge na makatibu wa bunge.

Amesema mfumo huo utakuwa ukitumika wakati wa vikao vya Bunge na kamati zake.

Akijibu maswali ya wabunge, Mtalaam wa Tehama wa Bunge Lilian Mraba amesema kwasasa mfumo huo utafanya kazi ndani ya viwanja vya Bunge.

Chanzo: mwananchi.co.tz