Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Vijana Chadema wamtaja Magufuli uchaguzi Serikali za mitaa

84304 Bavicha+pic Vijana Chadema wamtaja Magufuli uchaguzi Serikali za mitaa

Fri, 15 Nov 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam.  Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) limemuomba Rais wa Tanzania, John Magufuli kuzungumzia sintofahamu kuhusu uchaguzi wa Serikali za mitaa.

Limesema ukimya wake kuhusu uchaguzi huo unaogusa wananchi wengi utakaofanyika  Novemba 24, 2019 unatia shaka.

Vyama saba vya siasa; Chadema, ACT-Wazalendo, NLD,CUF,UPDP, Chauma na NCCR-Mageuzi  vimejitoa katika uchaguzi huo kwa madai ya kutotendewa haki ikiwa ni pamoja na wagombea wake kuenguliwa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Novemba 14, 2019 mwenyekiti wa Bavicha,  Patrick Ole Sosopi amesema kiongozi mkuu huyo wa nchi kunyamazia dhuluma wanazofanyiwa wananchi kunaashiria anafahamu kinachoendelea.

“Hatumlazimishi ila ajue kwamba Watanzania wamedhulumiwa haki zao hivyo azungumzie  mustakabali wa uchaguzi huu,” amesema Sosopi.

Baraza hilo limemtaka pia Waziri wa Tamisemi, Seleman Jafo kujiuzulu kwa madai ya kuuvuruga uchaguzi huo unaosimamiwa na wizara hiyo. Sosopi amedai Jafo ametoa kauli zinazoashiria ilipangwa uwe uchaguzi wa chama kimoja.

“Jafo anapaswa kujua kuwa ameshindwa kusimamia uchaguzi ajiuzulu na kama atashindwa kufanya hivyo, Bavicha tutamtaka rais amfute kazi,” amesema Sosopi.

Chanzo: mwananchi.co.tz