Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole leo Jumatano Machi 11, 2020 amefika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kulipa faini ya mwanachama wa chama hicho, Dk Vicent Mashinji.
Dk Mashinji na wanachama wanane wa Chadema jana Jumanne Machi 10, 2020 Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliwatia hatiani katika mashtaka 12 kati ya 13 yaliyokuwa yakiwakabili na kutakiwa kulipa faini ya jumla ya Sh350 milioni au kwenda jela miezi mitano
Katika faini hizo, Dk Mashinji anatakiwa kulipa Sh30 milioni.
Chadema wachangishana fedha usiku kuwatoa kina Mbowe rumande
MPYA: Mbowe, wenzake washindwa kulipa faini Sh350 milioni, kulala rumande