Baada ya aliyekuwa Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai kujiuzulu nafasi hiyo na kubaki kuwa Mbunge wa Jimbo la Kongwa, Mwananchi inakuletea baadhi ya kauli alizowahi kuzitoa ndani na nje ya Bunge hadi alipofikia kumwomba radhi Rais Samia Suluhu Hassan.
Baada ya aliyekuwa Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai kujiuzulu nafasi hiyo na kubaki kuwa Mbunge wa Jimbo la Kongwa, Mwananchi inakuletea baadhi ya kauli alizowahi kuzitoa ndani na nje ya Bunge hadi alipofikia kumwomba radhi Rais Samia Suluhu Hassan. Jana Alhamisi Januari 6, 2022 aliyekuwa Spika wa Bunge, Job Ndugai alitoa taarifa kwa umma kuwa amemuandikia barua Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya kujiuzulu nafasi hiyo.