Mon, 7 Feb 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mbunge wa Mtera (CCM), Livingstone Lusinde maarufu Kibajaji amesema kuna kampeni chafu kuelekea uchaguzi wa Naibu Spika wa Bunge, akidai kuwa zinalenga kuwagawa wabunge.
Kibajaji ametoa kauli hiyo nje ya viwanja vya Bunge leo Jumatatu Februari 7, 2022 wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mwenendo wa kampeni za wagombea wa nafasi ya Naibu Spika.
Jumla ya wabunge 11 wa CCM wamejitokeza kuomba kuteuliwa kukiwakilisha chama hicho kugombea nafasi ya unaibu Spika kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Dk Tulia Akson ambaye alichaguliwa kuwa Spika wa Bunge hilo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live