Rais Samia Suluhu Hassan amewataka wananchi na wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwa na umoja na upendo katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 ili wapate picha ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
“Tutakuwa na uchaguzi wa serikali za mitaa, niwaombe sana, muwaweke watu watakaowatumikia, tujitahidi sana kuepusha makundi, unapokosa tusitengeneze makundi.
“Dumisheni umoja na upendo ili uchaguzi huu utupe sura ya uchaguzi ujao wa mwaka 2025,”amesema.
Rais Samia ameyasema hayo leo Jumatatu Oktoba 16, 2023 katika hafla ya uzinduzi wa daraja la msingi mkoani humo ambapo yupo katika ziara ya kikazi.